Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo amewakabidhi Bodaboda wa Jiji la Arusha kiasi cha Shilingi 1,200,000 kwa ajili ya kutengeneza mfumo wa kuwezesha kusajili Bodaboda za Jiji la Arusha na kuwezesha upatikanaji wa taarifa za uhakika kwa ajili ya usalama na utalii.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi kiasi hicho, Gambo amesema kuwa yeye kama mbunge ni muhimu kutatua changamoto mbalimbali zinazowakumba anaowawakilisha, hivyo kukabidhi kiasi hicho ni moja ya njia za kutatua matatizo hayo.

“Mfumo huu ni kitu kizuri sana kwasababu unajua leo inaweza kutokea ajali ya bodaboda, pengine aliyepata ajali hali yake inaweza kuwa mbaya, akawa hawezi kuzungumza, unataka kumtafuta ndugu yake, taarifa unampataje? Lakini ndani ya mfumo, kuna taarifa za bodaboda na taarifa za wadhamini wake au ndugu zake”, amesema Gambo.

Nao viongozi wa Bodaboda Jiji la Arusha wakiwakilishwa na Mwenyekiti, Katibu na Mweka Hazina wamemshuru sana Gambo kwa kutatua changamoto zao kila wanapomfikishia na kuwaomba viongozi wengine waige mfano wake wa uongozi wenye kuacha alama.

“Mbunge wetu amekuwa akisaidia si tu Bodaboda, tunaona amekuwa akifanya mambo mengi kwenye vikundi mbalimbali, kwahiyo kazi anayoifanya tunaiona”, wameeleza.

About Author

Bongo News

2 Comments

    You have brought up a very good details, thankyou for the post.

    USDT娛樂城
    Maispin——2025年最新USDT娛樂城,安全、快速、刺激!
    歡迎來到 Maispin,2025年最具潛力的新秀 USDT娛樂城!在這裡,您只需提供 錢包地址 即可註冊,無需繁瑣的個人資訊,享受 安全、匿名、快速 的遊戲體驗。Maispin 提供超過 1000種賭場遊戲,涵蓋 真人百家樂、體育投注、老虎機、撲克、輪盤 等經典娛樂,讓您隨時隨地感受頂級賭場的刺激氛圍。我們與世界知名遊戲供應商合作,確保遊戲 公平公正,並提供高額彩金、獎勵活動,讓玩家輕鬆贏大獎!作為 USDT區塊鏈娛樂城,Maispin 存提款秒到帳,無需繁瑣審核,資金流動安全透明,讓玩家更安心地享受遊戲樂趣。立即加入 M宇宙,體驗前所未有的加密娛樂新潮流!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *