WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imedhamiria kuendelea kutatua changamoto za walimu zikiwemo za malimbikizo ya madeni na upandishaji wa madaraja.

Amesema kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anatambua, anathamini na kuheshimu kazi kubwa inayofanywa na walimu wote nchini katika kuhakikisha wanashiriki kikamilifu kukuza na kuiendeleza sekta ya elimu nchini.
Amesema hayo leo (Alhamisi, Desemba 12, 2024) alipomwakilisha Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa 19 wa Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari (TAHOSSA) uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Jakaya Kikwete jijini Dodoma
“Kwa sasa suala la stahiki za walimu linaendelea kuzingatiwa na Serikali imeendelea kufanya jitihada kubwa za kuhakikisha inapadisha madaraja watumishi walimu waliokosa na wanaopaswa kupandishwa, Serikali imedhamiria kuondoa msamiati wa areas (malimbikizo ya mishahara).”

Amesema kuwa katika kipindi cha (mwaka 2021/2022 hadi mwaka 2023/2024), Serikali imepandisha madaraja ya walimu 227,383 na kuwabadilishia miundo walimu 20,436.“ Ofisi ya Rais-TAMISEMI hakikisheni kila anaepanda daraja analipwa stahiki zake kwa wakati.”
Aidha, Waziri Mkuu amesema kuwa katika kipindi cha 2021/22 hadi 2023/24, jumla ya shilingi trilioni 1.76 zimetolewa na Serikali kwa ajili ya kuimarisha miundombinu ya shule ikiwemo ukarabati na ujenzi mpya.
“Miundombinu hii imesaidia kwa kiasi kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia, kupunguza msongamano wa wanafunzi madarasani na adha ya wanafunzi kutembea umbali mrefu kwenda shuleni.”

Akizungumzia kuhusu utekelezaji wa Sera ya Elimu bila Malipo, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Serikali imeendelea kutoa shilingi bilioni 33.3 kwa mwezi kwa ajili ya shule zote za Msingi na Sekondari za Serikali nchini ikiwa ni za uendeshaji wa shule pamoja na posho za madaraka.
“Wakati tunaanza mpango huu mwaka 2015/16 kila mwezi ilikuwa inatolewa shilingi bilioni 13.46, hivyo ongezeko hili ni sawa na asilimia 147.26. Utaratibu huu umekuwa chachu ya kuimarisha uandikishaji na mahudhurio ya wanafunzi katika ngazi mbalimbali.”
6 Comments
1вин вход http://1win104.com.kg/ .
1win kg https://www.1win105.com.kg .
служба поддержки мостбет номер телефона mostbet1009.com.kg .
mostbet casino mostbet casino .
мостбет кыргызстан скачать http://mostbet1000.com.kg .
娛樂城大解析
娛樂城,通常指的是一個線上賭博平台,提供各種娛樂遊戲,如賭場遊戲、體育博彩、電子遊戲等。這些平台讓玩家可以在網路上進行賭博,而不需要親自前往實體賭場。娛樂城通常包含了各式各樣的遊戲選項,例如百家樂、輪盤、老虎機、撲克等,並且透過即時娛樂、直播等技術,提升了玩家的沉浸感和互動性。現今的娛樂城大多數已經支援手機和桌面端的多平台操作,讓玩家可以隨時隨地參與遊戲,這樣的便利性使得它們受到全球玩家的青睞。此外,娛樂城也會推出不同的優惠活動、註冊獎金和忠誠計劃,吸引新用戶並保持老用戶的活躍度。然而,娛樂城的風險也不可忽視。由於賭博本身具有高度的娛樂性,但也存在可能的成癮問題。多數國家對於線上賭博有著嚴格的法律規範,玩家在選擇娛樂城平台時,應該格外留意平台的合法性和安全性,以避免陷入詐騙或遭遇其他法律風險。因此,理性投注並了解相關法律是每位玩家應該保持的基本態度。